skip to main |
skip to sidebar
KAJALA IS NOW FREE
STAA
wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja leo ameokolewa na Wema Sepetu
kwenda jela miaka mitano baada ya Wema kulipa faini ya milioni 13
aliyotakiwa kulipa Kajala,hukumu iliyotolewa leo jijini Dar Es Salaam na
Hakimu Mkazi Mahakama ya Kisutu .Aidha Mume wa Kajala Faraji Agustino
alitakiwa kulipa faini ya Milioni 200 au kwenda jela miaka 7.
Kajala alikuwa anakabiliwa na kesi ya kuuza nyumba iliyowekwa kizuizini
na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) baada ya mumewe,
Faraji Agustino kukumbwa na msala wa kutakatisha fedha haramu.
Awali mwaka jana Mwezi Machi,inadaiwa kuwa familia ya Kajala ilikataa
Wema kutoa fedha kwa ajili ya kumdhamini asiende jela lwa madai kuwa
walikuwa hawahitaji msaada kutoka kwa msanii mwenzake huyo.
No comments:
Post a Comment