September 11, 2013

OZIL AWASILI KAZINI ARSENAL, KUANZA MAZOEZI LEO
KIUNGO Mesut Ozil amewasili katika klabu yake mpya jana, Arsenal tayari kuanza kumtumikia Arsene Wenger anayekabiliwa na tatizo la wachezaji wengi majeruhi.
 
Mchezaji huyo aliyenunuliwa kwa Pauni Milioni 42 ataanza mazoezi leo makao makuu ya klabu, Colney London kwa mara ya kwanza tangu ahamie akitokea Real Madrid.
Na Wenger anajiandaa kumtumia mwanasoka huyo wa kimataifa wa Ujerumani katika mchezo dhidi ya Sunderland Jumamosi baada ya Tomas Rosicky kurejea kwenye mechi ya timu yake ya taifa akiwa majeruhi.
 
Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Jamhuri ya Czech aliumia wakati timu yake ikilala 2-1 dhidi ya Italia na yuko shakani kucheza Uwanja wa Light.
 
Hiyo inaacha milango wazi mno kwa Ozil kuanza kazi Arsenal, licha ya kwanza atakuwa na siku mbili tu kamili za kufanya mazoezi na wenzake kabla ya mechi hiyo.
 
Licha ya msimu kuwa umekwishaanza kwa karibu mwezi mzima, Arsenal tayari ina idadi kubwa ya majeruhi.
source: Sportmail

No comments: